WAZIRI WA FEDHA AIAGIZA NBAA KUANDAA WATAALAMU WENYE KUKIDHI MAHITAJI YA MAENDELEO YA TAIFA
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ameiagiza Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), kuhakikisha kuwa sekta ya uhasibu nchini inajengwa katika misingi imara ya maadili ili kuzalisha wataalamu wenye uadilifu, uwajibikaji na weledi unaokidhi mahitaji ya maendeleo ya Taifa.
Mhe. Balozi Omar alitoa maagizo hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Bodi hiyo ulioongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya NBAA, CPA Prof. Sylvia Temu, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha jijini Dar es Salaam, ambapo alipokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Taasisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/2026.
