WADAU JIJINI DAR ES SALAAM WASHIRIKI MAPITIO YA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA KUENDANA NA DIRA 2050.
Wizara ya Fedha imeendelea na mchakato wa kupitia upya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, kwa lengo la kuioanisha na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, kupitia kikao kazi kilichowakutanisha wadau mbalimbali kutoka sekta ya umma na binafsi.
Wizara imeendelea na mchakato huo ikiwa ni kikao kazi cha pili kufanyika ambapo wadau mbalimbali walipata fursa ya kutoa maoni na mapendekezo yatakayosaidia kuboresha Sheria hiyo, katika kikao kazi kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa Hazina, jijini Dar es Salaam.
